1Laiti ningekuwa, kama nilivyokuwa katika miezi iliyopita,
2Mungu alipoziangalia siku zangu!
3Hapo taa yake ilimulika juu ya kichwa changu, kwa mwanga wake nikaenda hata gizani.
18Kwa hiyo nilisema: Katika kiota changu ndimo, nitakamozimia, siku zangu zitakapokuwa nyingi kama za mtende.
19Mizizi yangu itatandama juu penye maji, nao umande utayanyea matawi yangu usiku kucha.
20Utukufu, nilio nao, utakuwa mpya kila siku, nao upindi wangu utajipatia nguvu mpya mkononi mwangu.
21Mimi watu walinisikiliza na kungoja, nimalize; nilipowapa shauri langu, wakaninyamazia.
22Hakuwako mwingine aliyesema, nilipokwisha kusema, maneno yangu yakawa kama matone yaliyowadondokea.
23Kama wanavyongoja mvua, ndivyo, walivyoningoja, vinywa vyao vikaasama kama vyao wanaotwetea mvua ya vuli.
24Walipotaka kukata tamaa, nikawachekea, hawakuweza kuuinamisha chini uso wangu, ulipoangaza.
25Nilipojielekeza kwenda kwao nilikaa nao kama kichwa chao, au kama mfalme katika vikosi vyake kwa kuwa kama mtu anayewatuliza mioyo waliosikitika.
Who We AreWhat We EelieveWhat We Do
2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.