1Ikawa, Sanibalati aliposikia, ya kuwa sisi tunalijenga boma, ndipo, makali yake yalipowaka moto, akakasirika sana, akawafyoza Wayuda.
16Tangu siku hiyo waliofanya kazi walikuwa nusu tu ya vijana wangu, nusu yao wengine walishika mikuki na ngao na pindi na shati zao za vyuma, nao wakuu wakawasimamia watu wote wa mlango wa Yuda,
17waliolijenga boma. Lakini wachukuzi waliopagaa mizigo kwa mkono mmoja wakafanya kazi, kwa mkono mwingine wakashika mata.
18Nao waliojenga kila mtu akawa amejifunga upanga wake kiunoni pake, naye mpiga baragumu akawa amesimama kando yangu.
19Nikawaambia wakuu wa miji na watawalaji na watu wengine wote pia: Hapa, tunapofanyia kazi zetu za kujenga, ni parefu mno, nasi tuko tumetawanyika ukutani, tunasimama mbali kidogo, kila mtu na mwenziwe;
20kwa hiyo hapo, mtakaposikia, baragumu likilia mahali, paendeeni, mkusanyike kwetu sisi! Naye Mungu wetu atatupigia vita hivi.
21Ndivyo, tulivyozifanya kazi zetu, nusu yao wakishika mikuki tangu hapo, jua lilipokucha, hata nyota zilipotokea.
22Hapo ndipo, nilipowaambia watu: Kila mtu na kijana wake sharti walale humu Yerusalemu, na usiku wawe walinzi, tena mchana wafanye kazi!
23Hapo wala mimi wala ndugu zangu wala vijana wangu wala walinzi walionifuata, sisi sote hatukuzivua nguo zetu; hata tulipokwenda mtoni, kila mtu alishika mata yake.
Who We AreWhat We EelieveWhat We Do
2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.