1Wewe Bwana hushinda, nikiulizana wa wewe; lakini na tusemeane hukumu zipasazo! Mbona njia zao wasiokucha huendelea vema, nao wadanganyifu wanaodanganya hutengemana?Mapatilizo na wokovu wa mataifa waliokaa na Wayuda.
14Hivi ndivyo, Bwana anavyosema kwa ajili ya wabaya wote, tuliokaa nao, waliolitwaa fungu lile, nililowapa wao walio ukoo wangu wa Isiraeli, liwe fungu lao: Wataniona, nikiwang'oa katika nchi yao, tena nikiwang'oa walio wa mlango wa Yuda katikati yao!
15Itakuwa, nitakapokwisha kuwang'oa nitawahurumia tena, niwarudishe kila mmoja penye fungu lake, kila mmoja katika nchi yake.
16Tena itakuwa, kama wale watajifundisha vema njia zao walio ukoo wangu, waape na kulitaja Jina langu na kusema: Hivyo, Bwana alivyo Mwenye uzima, kama wenyewe walivyowafundisha walio ukoo wangu kuapa na kumtaja Baali, basi, ndipo, watakapojengwa katikati yao walio ukoo wangu.Yer. 4:2; 5 Mose 6:13.
17Lakini kama hawasikii, nitaling'oa taifa hilo kabisa, liangamie; ndivyo, asemavyo Bwana.
Who We AreWhat We EelieveWhat We Do
2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.