1Yatawapata wanaowaza maovu,
watungao mabaya vitandani mwao,
wayafanye asubuhi kutakapopambazuka,
mikono yao ikiweza kuyamaliza.
2Kwa kutamani mashamba huyanyang'anya;
ikiwa nyumba, huzichukua nazo,
humkorofisha mwenye nyumba pamoja nao waliomo,
vilevile mwenye shamba, ijapo liwe fungu lake.
3Kweli hivi ndivyo, Bwana anavyosema:
Mtayaona mabaya, ninayouwazia mlango huu!
Yakiwapata, hamtaweza kuzitoa shingo zenu mle,
wala hamtaweza kwenda na kuzinyosha shingo zenu,
kwani siku hizo zitakuwa mbaya kweli.
4Siku hiyo watawatungia ninyi mfano,
wataomboleza ombolezo la kwamba:
Imefanyika! Tumeangamizwa!
Mafungu yao walio ukoo wangu anawapa wengine!
Kumbe mimi ameninyang'anya mashamba yetu,
awagawie wao wamkataao!
5Kwa hiyo hamtapata tena katika mkutano wa Bwana
atakayempimia mtu fungu, alilolipata kwa kura.
6Wao huhubiri: Msihubiri! Haifai kuhubiri mambo kama hayo, matusi nayo hayakomi!
13Mwenye kuwavunjia njia atawatangulia,
wapite langoni kwa kupavunja, watoke nje papo hapo;
ndipo, mfalme wao atakapowaongoza,
lakini atakayekwenda mbele yao wote ni Bwana.
Who We AreWhat We EelieveWhat We Do
2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.