1*Nawaonya, ndugu, kwa hivyo, Mungu alivyowaonea uchungu, mtoe miili yenu, iwe vipaji vitakatifu vya tambiko vyenye uzima vya kumpendeza Mungu; huko ndiko kumtumikia Mungu kunakoelekea.
3Kwa kipaji, nilichogawiwa, namwambia kila mmoja wa kwenu, asiwaze makuu yanayopapita hapo panapopasa kuwaza. Ila awaze, jinsi atakavyopata kuerevuka, kila mtu, kama Mungu alivyomgawia kumtegemea.
*Mwenye ufumbuaji sharti aupatanishe na kumtegemea Mungu.
7Mwenye utumishi sharti atumike kweli! Mfunzi na aushike ufundisho wake!Lipizi linalofaa.
17*Msimlipe mtu maovu kwa maovu! Yawazeni yaliyo mazuri mbele ya watu wote!Yes. 5:21; 1 Tes. 5:15.
18Kwa hivyo, mlivyo, mwe wenye kupatana na watu wote, ikiwezekana!Mar. 9:50; Ebr. 12:14.
19Wapendwa, msijilipize wenyewe, ila jitengeni, makali (ya Mungu) yapate kutokea! Kwani imeandikwa: Bwana anasema:
Lipizi ni langu mimi, ni mimi nitakayelipisha.
3 Mose 19:18; 5 Mose 32:35; Mat. 5:38-44.
20Lakini mchukivu wako akiwa ana njaa, mpe chakula!
Akiwa ana kiu, mpe cha kunywa!
Kwani ukivifanya hivyo,
utampalia makaa ya moto kichwani pake.Fano. 25:21-22; Mat. 5:44.
21Usishindwe nayo yaliyo maovu, ila maovu uyashinde kwa mema!*
Who We AreWhat We EelieveWhat We Do
2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.