Iyobu 41 - Swahili Roehl Bible 1937

Nguvu zake Nondo wa baharini (Lewiatani).

1Je? Unaweza kumvua nondo wa baharini kwa ndoana au kuufunga ulimi wake kwa kamba katika taya la chini?

12Sitanyamaza, nisiseme, jinsi viungo vyake vilivyo, nazo nguvu zake, jinsi zilivyo kubwa, nayo matengenezo yake, jinsi yalivyo mazuri.

13Yuko nani awezaye kulichuna vazi lake? Yuko nani atiaye mkono katika mataya yake yenye meno mawilimawili?

14Yuko nani awezaye kuifungua milango ya kinywa chake? Kwani pande zote zinayo meno yaogopeshayo.

15Magamba yake ni mazuri mno kwa hivyo, yanavyojipanga: kama ni kukazwa kwa nguvu ya chapa, hugandamana karibukaribu,

16hushikamana kabisa kila moja na mwenzake, upepo tu usiweze kupita katikati yao.

17Kweli kila moja linagandamana na mwenzake, yanashikana kwa nguvu, yasitengeke.

18Akienda chafya humulikisha mwanga, nayo macho yake yanafanana nayo makope ya mapambazuko.

19Mienge ya moto hutoka kinywani mwake, nayo hurukisha macheche ya moto.

20Katika mianzi ya pua yake hutoka moshi kama wa chungu kichemkacho au wa moto wa matete.

21Pumzi yake huunguza kama makaa yenye moto, hata miali ya moto hutoka kinywani mwake.

22Shingoni pake ndipo, nguvu zinapokaa, mbele yake yako matetemeko na mastusho.

23Manofu ya mwili wake yanashupaa, kwa kukazana hapo, yalipo, hayatikisiki.

24Moyo wake nao ni mgumu kama jiwe, ugumu wake ni kama wa jiwe la chini la kusagia.

25Akiinuka, nao wenye nguvu hushikwa na woga, kwa kustushwa hukosa njia ya kukimbilia.

26Ukimpiga kwa upanga haumwingii, wala mkuki wala mshale wala chuma cho chote.

27Chuma hukiwazia kuwa jani kavu, nayo shaba huiwazia kuwa mti uliobunguka.

28Mishale ya upindi haiwezi kumkimbiza, nayo mawe ya kombeo kwake hugeuka kuwa kama makapi.

29Marungu huwaziwa naye kuwa mabua makavu, tena huicheka shindo ya mkuki, ukitupwa.

30Upande wake wa chini una vigae vyenye pembe, alipogaagaa ni kama matopeni, palipopita gari la kupuria.

31Hukichafua nacho kilindi, kiwe kama chungu kinachochemka; huivuruga nayo bahari, iwe kama dawa, zikivurugwa chunguni.

32Nyuma yake hiyo njia, aliyoishika, huangazika, hilo povu la kilindi mtu angeliwazia kuwa mvi.

33Huku nchini hakuna afananaye naye; alichoumbiwa, ni hiki: asistuke kamwe!

34Wote walio wakuu huwatazama tu, kuliko wenye majivuno wote mfalme ndiye yeye.

Iyobu anajuta.

Iyobu akamjibu Bwana akisema:

Blog
About Us
Message
Site Map

Who We AreWhat We EelieveWhat We Do

Terms of UsePrivacy Notice

2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.

Home
Gospel
Question
Blog
Help