Mashangilio 116 - Swahili Roehl Bible 1937

Kuushukuru wokovu wa Mungu.

1Nampenda Bwana, kwa kuwa husikia, huisikia sauti yangu, nikimlalamikia.

2Kwa kuwa hunitegea nami sikio lake, kwa hiyo nitamwitia siku zangu zote.

3Matanzi ya kifo yalikuwa yameninasa, masongano ya kuzimu yakanipata, kwa kuona masikitiko nikasongeka.

12Nitawezaje kumrudishia Bwana mema yote, aliyonitendea?

13Nitakiinua kinyweo chenye wokovu, kisha nitalitambikia Jina lake Bwana.

15Ni jambo kuu machoni pa Bwana, wamchao wakifa.Sh. 72:14.

16Mimi nakuomba, Bwana, mimi mtumishi wako, mimi mtumishi wako ni mwana wa mjakazi wako, nawe umenifungulia mafungo yangu.

17Nitakutolea wewe vipaji vya tambiko vya kukushukuru, kisha nitalitambikia Jina lake Bwana.

18Nitamlipa Bwana, niliyomwapia, wote walio ukoo wake wavione na macho yao,

19katika nyua zake Nyumba ya Bwana, katikati mjini mwako, wewe Yerusalemu. Haleluya!

Blog
About Us
Message
Site Map

Who We AreWhat We EelieveWhat We Do

Terms of UsePrivacy Notice

2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.

Home
Gospel
Question
Blog
Help