Mifano 5 - Swahili Roehl Bible 1937

Msizini!

1Mwanangu, usikilize werevu wangu ulio wa kweli!

Utegee utambuzi wangu sikio lako,

2upate kuyaangalia mawazo ya moyo,

midomo yako nayo iulinde ujuzi!

3Kwani midomo ya mwanamke mgeni hudondosha asali,

kinywa chake nacho huteleza kuliko mafuta.

20Mwanangu, mbona unataka kujilewesha kwa mwanamke mgeni?

Mbona unataka kukumbatia kifua cha mwanamke wa mwingine?

21Kwani machoni pa Bwana njia za kila mtu ziko waziwazi,

yeye ndiye anayeyatengeneza mapito ya kila mtu.

22Manza, alizozikora mwenyewe, zitamnasa asiyemcha Mungu,

akamatwe na kamba za makosa yake.

23Huyo atakufa, kwa kuwa hakuonyeka,

kwa ujinga wake mwingi atapepesuka, aanguke.

Blog
About Us
Message
Site Map

Who We AreWhat We EelieveWhat We Do

Terms of UsePrivacy Notice

2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.

Home
Gospel
Question
Blog
Help