1Ahaswerosi alikuwa akitawala majimbo 127 kutoka nchi ya Uhindi mpaka nchi ya Nubi. Ikawa katika siku zake Ahaswerosi
2hapo, yeye mfalme Ahaswerosi alipokaa katika kiti chake cha kifalme jumbani mwake huko Susani,
3katika mwaka wa tatu wa ufalme wake ndipo, alipowafanyia wakuu wake wote pamoja na watumishi wake karamu kubwa. Wakawako mbele yake wakuu wa vikosi vya Persia nao vya Media, hata wenye macheo na wakuu wa majimbo.
4Akawaonyesha mali na malimbiko ya ufalme wake nayo marembo na utukufu wake mwingi siku nyingi, yaani siku 180.
5Siku hizo zilipokwisha kupita, mfalme akawafanyia watu wote pia waliopatikana mle Susani penye jumba lake, wakubwa kwa wadogo, karamu ya siku saba uani penye bustani ya jumba la mfalme.
6Mazulia meupe na meusi mazuri mno yalikuwa yamefungwa kwa kamba za pamba nyeupe na nyekundu katika pete za fedha penye nguzo za mawe meupe. Nayo magodoro ya kukalia yaliyofumwa kwa nyuzi za dhahabu na za fedha yalikuwa yametandikwa sakafuni palipotengenezwa kwa mawe mekundu na meupe na ya manjano na meusi.
7Vyombo, watu walivyovipata vya kunywea, vilikuwa vya dhahabu; hivyo vyombo navyo vilipitanapitana kwa namna zao, nazo mvinyo za kifalme zilikuwa nyingi, kama inavyoupasa utu wa mfalme.
8Kama ilivyoagizwa, watu wakanywa, kama walivyotaka pasipo kushurutishwa; kwani nidvyo, mfalme alivyowaagiza wakuu wote wa nyumbani mwake, waache, kila mtu anywe, kama anavyopendezwa.
9Naye Wasti, mkewe mfalme, alifanya karamu ya wanawake mle ndani ya jumba la kifalme la mfalme Ahaswerosi.
10Siku ya saba, moyo wa mfalme ulipochangamshwa na mvinyo, akawaambia akina Mehumani, Bizita, Harbona, Bigita, Abagita, zetari, na Karkasi, watumishi wake saba wa nyumbani waliomtumikia mfalme Ahaswerosi mwenyewe,
11wamlete Wasti mkewe mfalme, amtokee mfalme na kuvaa kilemba cha kifalme, awaonyeshe watu wote nao wakuu uzuri wake, kwani alikuwa kweli mwenye sura nzuri.
12Lakini Wasti, mkewe mfalme, akakataa kuja kwa ile amri, mfalme aliyompelekea kwa vinywa vya wale watumishi wa nyumbani. Ndipo, mfalme alipokasirika sana, makali yake yakawaka moto moyoni mwake.
13Basi, mfalme akafanya shauri na mafundi wa kuvijua vielekezo vya siku, kwani ilikuwa desturi yake mfalme kuulizana nao wote waliozijua amri na hukumu za serikali.
Who We AreWhat We EelieveWhat We Do
2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.