1Bwana, gombana nao wanigombezao! Pigana nao wanipiganishao!
2Shika ngao na kingio! Inuka, unisaidie!
17Bwana, utawatazama tu mpaka lini? Irudishe roho yangu uzimani, wasiimalize! Nitoe kwenye wana wa simba! Kwani niko peke yangu.
22Bwana, umeyaona, usiyanyamazie! Usinikalie mbali, Bwana wangu!
23Amka! Inuka, uniamulie! Mungu wangu na Bwana wangu, unigombee!Sh. 44:24.
24Niamulie kwa wongofu wako, Bwana Mungu wangu, wasinifurahie!
25Wasiseme mioyoni mwao: Weye! Ndivyo vinavyotupendeza! Wala wasiseme: Tumemmeza!
26Sharti watwezwe wakiumbuliwa wote pamoja waliofurahiwa na mabaya yaliyonipata, sharti wavikwe soni, nyuso ziwaive waliojikuza na kuninyenyekeza.Sh. 35:4.
27Lakini wao waliopendezwa na wongofu wangu sharti wapige vigelegele kwa kufurahiwa! Sharti waseme pasipo kukoma: Mkuu ni Bwana, mtumishi wake akikaa na kutengemana, hupendezwa.Sh. 40:17.
28Ulimi wangu sharti uusimulie wongofu wako, ukusifu wewe siku zote!
Who We AreWhat We EelieveWhat We Do
2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.