1Mungu, piga mbio, uniopoe! Bwana, pigambio, unisaidie!Sh. 38:1.
2Sharti wapatwe na soni wakiumbuliwa walioitafuta roho yangu. Sharti warudishwe nyuma na kutwezwa wao waliopendezwa na mabaya yaliyonipata mimi.
3Sharti warudi nyuma na kuona soni wale walioniambia: Weye! Weye!
4Sharti wachangamke na kufurahiwa wote wakutafutao! Waupendao wokovu wako waseme pasipo kukoma: Mkuu ni Mungu!
5Nami mnyonge, hata mkiwa; Mungu, piga mbio, unijie! Msaada wangu na wokovu wangu ndiwe wewe; wewe Bwana, usinikawilie!
Who We AreWhat We EelieveWhat We Do
2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.