1Naikweza roho yangu, ikuelekee Bwana.
2Mungu wangu, nimekutegemea, sitapatwa na soni, adui zangu wasipate kushangilia kwa ajili yangu mimi.
3Hawatapatwa na soni kabisa wote wakungojeao, watakaopatwa na soni ndio wakupingao bure.
8Bwana ni mwema na mwongofu; kwa hiyo huonya wakosaji, wakiwa njiani bado.
9Huongoza wanyonge, wakiamuliwa, kweli hufundisha wanyonge njia yake.
10Penya upole na kweli ndipo pote, Bwana anapotangulia, kwao walishikao Agano lake nayo mashuhuda yake.
11Kwa ajili ya Jina lako, Bwana, niondolee manza, kwani hizo, nilizozikora, ni nyingi mno.
Who We AreWhat We EelieveWhat We Do
2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.