Yesaya 52 - Swahili Roehl Bible 1937

Wokovu wa Sioni.

1Amka! Amka! Ivae nguvu yako, Sioni!

Zivae nguo zako tukufu, Yerusalemu, ulio mji mtakatifu!

Kwani mwako hatamwingia tena

asiyetahiriwa wala mwenye uchafu.

2Yakung'ute mavumbi, kisha inuka, upate kukaa, Yerusalemu!

Yafungue mafungo yaliyopo shingoni pako,

binti Sioni, uliofungwa!

3Kwani hivi ndivyo, Bwana anavyosema: Mliuzwa bure, kwa hiyo hamtakombolewa kwa fedha.

8Zisikilize sauti za walinzi wako!

Wamepaza sauti pamoja na kupiga shangwe,

kwani wanaona na macho yao, Bwana akirudi Sioni.

9Pigeni shangwe na kupaza sauti,

ninyi mabomoko ya Yerusalemu!

Kwani Bwana amewatuliza mioyo walio ukoo wake,

akaukomboa Yerusalemu.

10Mkono wake mtakatifu Bwana ameuvua nguo

machoni pa makabila yote ya watu,

mapeo yote ya nchi yauone wokovu wa Mungu wetu.*

11Ondokeni! Ondokeni! Tokeni hapa! Msiguse yenye uchafu!

Tokeni humu kati! Jitakaseni, ninyi

mnaovichukua vyombo vya Bwana!

12Kwani hamtatoka upesiupesi,

wala hamtakwenda na kukimbia,

kwani atakayewaongoza ni Bwana,

naye atakayewakusanya nyuma ni Mungu wa Isiraeli.

13Mtazameni mtumishi wangu,

jinsi atakavyoendelea kwa welekevu:

atatukuka na kukwezwa, awe mkuu kabisa!

14Kama wengi walivyokustuka, watamstuka naye:

kwa kuwa walipomtazama alikuwa amenyongeka kuliko watu,

nalo umbo lake halikuwa kama la wana wa watu;

15ndivyo, atakavyoshangaza makabila mengi ya watu,

nao wafalme wafumbe vinywa vyao kwa ajili yake yeye;

kwani watakaomwona ndio wasioambiwa Neno lake,

nao wasiolisikia watalijua maana.

Blog
About Us
Message
Site Map

Who We AreWhat We EelieveWhat We Do

Terms of UsePrivacy Notice

2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.

Home
Gospel
Question
Blog
Help