1Mungu, wamizimu wameuingia mji ulio fungu lako, wakalichafua Jumba lako lililo takatifu, Yerusalemu wakaugeuza kuwa mabomoke tu.
2Mizoga ya watumishi wako wameitoa, iliwe na ndege wa angani, nayo miili yao wlaiokucha wamewapa nyama wa porini.
3Damu zao wakazimwaga kama maji, zizunguke Yerusalemu, tena hakuna aliyewazika hao waliokufa.
4Majirani zetu tunaona soni kwao, maana watuzungukao wanatufyoza na kutusimanga.
5Bwana, mpaka lini utatukasirikia? Itakuwa kale na kale? Wivu wako unachoma kama moto uwakao.
13Ndipo, sisi tulio ukoo wako na kindoo, unaowachunga, tukapokutolea shukrani kale na kale, tukisimulia vizazi na vizazi, ya kuwa inapasa kukushangilia.
Who We AreWhat We EelieveWhat We Do
2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.