1Ikawa katika mwaka wa 4 wa Yoyakimu, mwana wa Yosia, mfalme wa Yuda, ndipo, neno hili lilipomjia Yeremia likitoka kwa Bwana kwamba:
30Kwa hiyo Bwana anasema hivi kwa ajili ya Yoyakimu, mfalme wa Yuda: Hatampata atakayekaa katika kiti cha kifalme cha Dawidi, nao mzoga wake utakuwa umetupiwa jua kali la mchana nayo baridi ya usiku.Yer. 22:19.
31Nitampatilizia yeye na kizazi chake na watumishi wake manza zao, walizozikora, nikiwaletea wao nao wakaao Yerusalemu nao watu wa Yuda mabaya yote, niliyoyasema, ya kuwa nitawafanyizia, lakini hawakusikia.
32Ndipo, Yeremia alipochukua kitabu kingine cha kuzingwa, akampa mwandishi Baruku, mwana wa Neria, akayaandika humo, Yeremia aliyoyasema kwa kinywa chake, ni maneno yote ya kile kitabu, Yoyakimu, mfalme wa Yuda, alichokiteketeza kwa moto, pakaongezwa tena maneno mengi kama hayo.
Who We AreWhat We EelieveWhat We Do
2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.