Mika 3 - Swahili Roehl Bible 1937

Mapatilizo yao wakuu.

1Nikasema: Sikilizeni, ninyi mlio vichwa vyao wa Yakobo,

ninyi mlio wakuu wa mlango wa Isiraeli!

Je? Haiwapasi ninyi kujua, jinsi mashauri yanavyokatwa

sawasawa?

2Lakini ninyi huchukizwa nayo yaliyo mema,

mkapendezwa nayo yaliyo mabaya;

ninyi huchuna watu ngozi zao,

nazo nyama zao huziondoa mifupani kwao.

3Ninyi ndio mnaozila nyama zao walio ukoo wangu,

tena mkiisha kuwavua ngozi zao mwawavunja nayo mifupa

yao,

mkawakatakata vipande kama vya kuweka chunguni

au kama nyama zinazotiwa katika sufuria.

4Kwa hiyo hapo, watakapomlilia Bwana, hatawaitikia,

ila atauficha uso wake, usiwatazame wakati huo,

kama inavyowapasa kwa matendo yao mabaya, waliyoyafanya.

5Hivi ndivyo, Bwana anavyosema kwa ajili ya wafumbuaji

wanaowapoteza walio ukoo wangu,

ndio wanaotangaza kwamba: Tengemaneni tu!

wakipata vya kutafuna kwa meno yao,

lakini mtu asipowapa vya kutia vinywani mwao,

humpatia vita vya watakatifu

6Kwa hiyo usiku utawaguia, msione kitu,

na giza, msiweze kuagua,

nalo jua litawachwea wafumbuaji hao,

hata siku itakuwa yenye giza kwao.

7Ndipo, hao wachunguzaji watakapopatwa na soni,

nao waaguaji hao wataiva nyuso,

wao wote watajifunika ndevu zao za midomo,

kwa kuwa Mungu hawajibu kamwe.

8

11Wakuu wao hukata mashauri kwa kupenyezewa mali,

nao watambikaji wao hufundisha kulipwa,

nao wafumbuaji wao hufumbua kwa kupata fedha,

tena hujiegemezea kwake Bwana na kusema:

Je? Bwana hayuko kwetu katikati?

Hakuna kibaya kitakachotupata.

12Kweli kwa ajili yenu ninyi Sioni utalimwa kuwa shamba,

nao Yerusalemu utageuka kuwa chungu la mabomoko,

nao mlima wenye Nyumba hii utageuka kuwa kilima chenye

mwitu.

Blog
About Us
Message
Site Map

Who We AreWhat We EelieveWhat We Do

Terms of UsePrivacy Notice

2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.

Home
Gospel
Question
Blog
Help