1Yatakayowapata wana wa Amoni. Hivi ndivyo, Bwana anavyosema: Je? Hakuna wana kwao Waisiraeli? Hakuna awezaye kulichukua fungu lake? Mbona Malkamu ameichukua nchi ya Gadi nao watu wa ukoo wake wanakaa katika miji yao?Mapatilizo ya Waedomu.
7Yatakayowapata Waedomu. Hivi ndivyo, Bwana Mwenye vikosi anavyosema: Je? Huko Temani hakuna tena werevu wa kweli? Wajuzi wamepotelewa na akili, werevu wao wa kweli ukatoweka?Mapatilizo ya Waelamu.
34Hili ndilo neno la Bwana lililomjia mfumbuaji Yeremia kuwaambia Waelamu, Sedekia, mfalme wa Yuda, alipoanzia kuwa mfalme.
35Hivi ndivyo, Bwana Mwenye vikosi anavyosema: Mtaniona, nikizivunja pindi zao Waelamu, nguvu zao nyingi zilimo.
36Nitawaletea Waelamu pepo nne zitokazo pande nne za mbinguni, niwatawanye kwenye hizo pepo, pasiwe taifa lisilojiwa na watoro wa nchi ya Elamu.
37Nitawastusha Waelamu, wawaogope adui zao nao wazitafutao roho zao; kisha nitawaletea mabaya, makali yangu yenye moto yatakapowawakia, mpaka niwamalize.
38Ndipo, nitakapokiweka kiti changu cha kifalme huko Elamu, nimwangamize mfalme na wakuu, watoweke huko; ndivyo, asemavyo Bwana.
39Lakini siku zitakapotimia, nitayafungua mafungo ya Waelamu; ndivyo, asemavyo Bwana.
Who We AreWhat We EelieveWhat We Do
2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.