Mashangilio 122 - Swahili Roehl Bible 1937

Kuuombea Yerusalemu.Wimbo wa Dawidi wa kupapandia Patakatifu.

1*Niliwafurahia walioniambia: Twende Nyumbani kwa Bwana!Sh. 26:6-8.

2Hivyo miguu yetu iko ikisimama malangoni kwako, Yerusalemu.

3Yerusalemu umejengwa tena kama mji ulioungamanishwa vema.

4Ndiko, mashina ya watu yanakopanda, yaliyo mashina ya Bwana; ndiko, wanakowashuhudia Waisiraeli, walishukuru Jina la Bwana.

5Kwani viti vya uamuzi vilipowekwa, ndipo pale, ni viti vya kifalme vya mlango wa Dawidi.

6Uombeeni Yerusalemu utengemano, watengemane nao waupendao!Zak. 4:7.

7Sharti uwe utengemano ndani ya boma lako, nao utulivu katika majumba yako yaliyo mazuri mno.

8Kwa ajili yao walio ndugu zangu na rafiki zangu na niseme tena na kuomba: Utengemano na uwe kwako!

9Kwa ajili ya Nyumba ya Bwana Mungu wetu na nikutafutie mema.*

Blog
About Us
Message
Site Map

Who We AreWhat We EelieveWhat We Do

Terms of UsePrivacy Notice

2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.

Home
Gospel
Question
Blog
Help