Mifano 24 - Swahili Roehl Bible 1937

Vumilia na kupatana!

1Usione wivu kwa ajili ya watu wabaya,

wala usitamani kuwa mwenzao!

2Kwani mioyo yao huwaza mwangamizo,

nayo midomo yao husema makorofi.

3Nyumba hujengwa kwa werevu wa kweli

ikishikizwa kwa utambuzi.

4Kwa ujuzi vyumba vyake hujazwa

vitu vyote vyenye kima vipendezavyo.

13Mwanangu, ule asali, kwani ni njema,

ile asali iliyo safi yenyewe, kwani ni tamu, ukiitia kinywani.

14*Nao werevu wa kweli uujue, ya kuwa ni utamu wa roho;

ukiupata, basi, mwisho utafanikiwa,

nacho kingojeo chako hakitang'oleka.

15Wewe usiyemcha Mungu, usiotee penye kao la mwongofu,

wala usipabomoe pake pa kulalia!

16Kwani mwongofu akianguka mara saba huinuka,

lakini wasiomcha Mungu hujikwaza penye mabaya.

23Mifano hii nayo ilitoka kwa watu werevu wa kweli.

Upendeleo haufai kabisa shaurini.

27Fanya kazi zako za huko nje, kajitengenezee mashamba yako,

kisha jijengee nyumba yako!

28Usiwe shahidi ya kumshinda mwenzio bure!

Je? Huko hutadanganya kwa midomo yako?

30Nilipopita penye shamba la mvivu

napo penye mizabibu ya mtu aliyepotelewa na akili,

31nikapaona, pote palikuwa miiba tu,

pote palikuwa pamefunikwa na viwawi,

nacho kitalu chake cha mawe kilikuwa kimebomoka.

32Nilipoyaona nikayashika na kuyaweka moyoni mwangu mimi,

niyatumie ya kunionya.

33Ukitaka kulala bado kidogo na kupumzika bado kidogo

na kukunja mikono kitandani bado kidogo,

Blog
About Us
Message
Site Map

Who We AreWhat We EelieveWhat We Do

Terms of UsePrivacy Notice

2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.

Home
Gospel
Question
Blog
Help