1Usione wivu kwa ajili ya watu wabaya,
wala usitamani kuwa mwenzao!
2Kwani mioyo yao huwaza mwangamizo,
nayo midomo yao husema makorofi.
3Nyumba hujengwa kwa werevu wa kweli
ikishikizwa kwa utambuzi.
4Kwa ujuzi vyumba vyake hujazwa
vitu vyote vyenye kima vipendezavyo.
13Mwanangu, ule asali, kwani ni njema,
ile asali iliyo safi yenyewe, kwani ni tamu, ukiitia kinywani.
14*Nao werevu wa kweli uujue, ya kuwa ni utamu wa roho;
ukiupata, basi, mwisho utafanikiwa,
nacho kingojeo chako hakitang'oleka.
15Wewe usiyemcha Mungu, usiotee penye kao la mwongofu,
wala usipabomoe pake pa kulalia!
16Kwani mwongofu akianguka mara saba huinuka,
lakini wasiomcha Mungu hujikwaza penye mabaya.
23Mifano hii nayo ilitoka kwa watu werevu wa kweli.
Upendeleo haufai kabisa shaurini.
27Fanya kazi zako za huko nje, kajitengenezee mashamba yako,
kisha jijengee nyumba yako!
28Usiwe shahidi ya kumshinda mwenzio bure!
Je? Huko hutadanganya kwa midomo yako?
30Nilipopita penye shamba la mvivu
napo penye mizabibu ya mtu aliyepotelewa na akili,
31nikapaona, pote palikuwa miiba tu,
pote palikuwa pamefunikwa na viwawi,
nacho kitalu chake cha mawe kilikuwa kimebomoka.
32Nilipoyaona nikayashika na kuyaweka moyoni mwangu mimi,
niyatumie ya kunionya.
33Ukitaka kulala bado kidogo na kupumzika bado kidogo
na kukunja mikono kitandani bado kidogo,
Who We AreWhat We EelieveWhat We Do
2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.