1Siku hiyo mfalme Ahaswerosi akampa Esteri, mkewe mfalme, nyumba ya Hamani, aliyekuwa mpingani wao Wayuda. Mordekai akaja kwa mfalme, kwani Esteri alimsimulia mfalme, udugu wao ulivyo.
2Ndipo, mfalme alipoondoa kidoleni pete yake yenye muhuri, aliyomvua Hamani, akampa Mordekai. Naye Esteri akamkalisha Mordekai katika nyumba ya Hamani.
3Esteri akaendelea kusema mbele ya mfalme, akamwangukia miguuni na kulia machozi na kumlalamikia, autangue ule ubaya wa Hamani wa Agagi nayo mashauri yake, aliyowatakia Wayuda.
4Mfalme alipompungia Esteri kwa bakora yake ya dhahabu, Esteri akainuka, asimame mbele ya mfalme,
Who We AreWhat We EelieveWhat We Do
2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.