5 Mose 27 - Swahili Roehl Bible 1937

Mawe ya kuwakumbushia Waisiraeli Maonyo.

1Mose pamoja na wazee wa Waisiraeli wakawaagiza watu kwamba: Yaangalieni maagizo yote, mimi ninayowaagiza leo!

16Na awe ameapizwa atakayembeza baba yake na mama yake! Nao watu wote na waitikie: Amin!

17Na awe ameapizwa atakayeusogeza mpaka wa mwenzake! Nao watu wote na waitikie: Amin!

18Na awe ameapizwa atakayempoteza kipofu njiani! Nao watu wote na waitikie: Amin!

19Na awe ameapizwa atakayepotoa shauri la mgeni au la mwana aliyefiwa na wazazi au la mjane! Nao watu wote na waitikie: Amin!

20Na awe ameapizwa atakayelala na mkewe baba yake! Kwani huko atazifunua nguo za baba yake. Nao watu wote na waitikie: Amin!

24Na awe ameapizwa atakayempiga mwenzake mahali panapojificha! Nao watu wote na waititike: Amin!

25Na awe ameapizwa atakayechukua mapenyezo, ampige mtu na kuimwaga damu yake asiyekosa! Nao watu wote na waitikie: Amin!

26Na awe ameapizwa asiyeyasimamisha maneno ya Maonyo haya na kuyafanya! Nao watu wote na waitikie: Amin!

Blog
About Us
Message
Site Map

Who We AreWhat We EelieveWhat We Do

Terms of UsePrivacy Notice

2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.

Home
Gospel
Question
Blog
Help