1Wasiomcha Mungu hukimbia pasipo kufukuzwa,
lakini waongofu hutulia pasipo kustushwa kama mwana wa simba.
2Kwa ajili ya mapotovu ya nchi wakuu wake huwa wengi,
lakini mtambuzi mwenye akili huitengemanisha siku nyingi.
3Mtu akosaye mali akikorofisha wanyonge,
ni mvua ifurikayo pasipo kuleta chakula.
4Wayaachao Maonyo huwasifu wasiomcha Mungu,
lakini wayaangaliao Maonyo huwakasirisha sana.
Who We AreWhat We EelieveWhat We Do
2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.