1Adamu akamtambua mkewe Ewa, akapata mimba; kisha akamzaa Kaini, akasema: Nimepata mwanamume kwa Bwana.
2Tena akamzaa ndugu yake Abeli; naye Abeli akawa mchunga kondoo, lakini Kaini akawa mlima shamba.
3Siku zilipopita, Kaini akampelekea Bwana mazao ya shamba kuwa kipaji cha tambiko.
4Abeli naye akapeleka malimbuko ya kundi lake yenye manono. Bwana akamtazama Abeli na kipaji chake kwa kupendezwa,Kaini anamwua nduguye Abeli.
8Kisha Kaini akaongea na nduguye Abeli; lakini walipofika shambani, ndipo, Kaini alipomwinukia nduguye Abeli, akamwua.Kuzaliwa kwake Seti.
25Adamu alipomtambua mkewe tena, akazaa mwana wa kiume, akamwita jina lake Seti (Pato), kwani alisema: Mungu amenipatia mzao mwingine mahali pake Abeli, kwa kuwa kaini alimwua.
26Seti naye alipozaliwa mwana akamwita jina lake Enosi. Siku hizo ndipo, watu walipoanza kulitambikia Jina la Bwana.
Who We AreWhat We EelieveWhat We Do
2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.