Mifano 7 - Swahili Roehl Bible 1937

Jinsi majaribu ya uzinzi yanavyoponza watu.

1Mwanangu, yaangalie maneno yangu,

uyashike sana maagizo yangu moyoni mwako!

2Yaangalie maagizo yangu! Ndipo, utakapopata uzima;

yaangalie maonyo yangu, kama unavyoangalia mboni ya jicho lako!

3Yafunge vidoleni pako,

tena yaandike katika kibao cha moyo wako!

6Kwani dirishani nyumbani mwangu

siku moja nilipochungulia penye vyuma vyake,

7niliwatazama wajinga, nikaona kijana mmoja aliyepotelewa na akili,

nikamtambua katikati yao wasioyajua bado mambo hayo.

8Alitembea barabarani hapo pembeni, yule alipokaa,

akaishika njia ya kutembea penye nyumba yake;

9ikawa jioni, jua lilipokwisha kuchwa,

hata ikawa usiku wa manane penye giza.

10Mara mwanamke anakuja kukutana naye,

alivaa nguo kama mgoni, nao moyo wake ulikuwa mdanganyifu.

11Anapiga kelele pasipo kujizuia,

miguu yake haipendi kukaa nyumbani mwake;

12mara moja yuko barabarani, mara nyingine yuko uwanjani,

huvizia po pote penye njia panda.

13Basi, huyu akamshika, akamnonea,

akaushupaza uso wake akamwambia:

14Sina budi kutoa kipaji cha tambiko cha shukrani,

leo hivi ninavilipa viapo vyangu.

Blog
About Us
Message
Site Map

Who We AreWhat We EelieveWhat We Do

Terms of UsePrivacy Notice

2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.

Home
Gospel
Question
Blog
Help