Mashangilio 102 - Swahili Roehl Bible 1937

Kuomba kwa mnyonge, Sioni ujengwe tena.(Wimbo wa juto wa 5.)

1Maombo ya mnyonge; kwa kufikisha kuzimia roho anamtolea Bwana wasiwasi wake.

2Bwana, lisikilize ombo langu! Kilio changu sharti kifike kwako wewe.

3Usiufiche uso wako, nisiuone ninaposongeka! Nitegee sikio lako, ninapokuita, uniitikie upesi!

4Kwani siku zangu hupotea kama moshi, nayo mifupa yangu huchomwa kama vijinga vya moto.

5Moyo wangu umeungua, ukanyauka kama majani, kwa hiyo mimi husahau kula chakula changu.

6Kwa hivyo, ninavyolia na kupiga kite, nyama za mwili wangu zimegandamana nayo mifupa.

24Njiani alizipunguza nguvu zangu, nazo siku zangu akazifupiza.

25Nikasema: Mungu wangu, usiniondoe, siku zangu simefika kati tu! Miaka ikaayo kwa vizazi na vizazi ni yako wewe.

Blog
About Us
Message
Site Map

Who We AreWhat We EelieveWhat We Do

Terms of UsePrivacy Notice

2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.

Home
Gospel
Question
Blog
Help