1Bwana akawambia Mose na Haroni kwamba:
14Nayo haya maonyo sharti yaangaliwe, mtu akifa hemani: kila atakayeingia humo hemani naye kila atakayekuwamo humo hemani atakuwa mwenye uchafu siku saba.
15Nacho kila chombo kilicho wazi kisichofunikwa na kifuniko cha kukifungia kabisa ni chenye uchafu.
16Hata kila mtu atakayegusa porini mtu aliyeuawa kwa upanga au mfu au mfupa wa mtu au kaburi atakuwa mwenye uchafu siku saba.
17Mtu akiwa mwenye uchafu hivyo, na wachukue majivu machache ya hiyo ng'ombe ya weuo iliyoteketezwa, wayatie chomboni, kisha watie humo maji ya mtoni.
18Kisha mtu mwenye kutakata na achukue kivumbasi, akichovye katika hayo maji, ayanyunyizie lile hema na vyombo vyote vilivyomo nao watu wote waliokuwamo naye yule mtu aliyegusa mfupa wa mzoga wa mtu aliyeuawa kwa upanga au mfu au kaburi.
19Ndivyo, mwenye kutakata atakavyomnyunyizia mwenye uchafu siku ya tatu na siku ya saba; akiisha kumweua hiyo siku ya saba sharti azifue nguo zake pamoja na koga majini, ndivyo, atakavyokuwa jioni mwenye kutakata.
20Lakini mtu akiwa mwenye uchafu pasipo kujieua, basi, aliye hivyo hana budi kung'olewa katika mkutano huu, kwani hupachafua Patakatifu pa Bwana, kwani asiponyunyiziwa hayo maji ya kunyunyiza, ni mwenye uchafu vivyo hivyo.
21Haya yawe kwao maongozi ya kale na kale. Naye yule aliyemnyunyizia mwenzake hayo maji ya kunyunyiza sharti azifue nguo zake. Naye atakayeyagusa hayo maji ya kunyunyiza atakuwa mwenye uchafu mpaka jioni.
22Navyo vyote, mwenye uchafu atakavyovigusa, vitakuwa vyenye uchafu, naye kila mtu, atakayemgusa, atakuwa mwenye uchafu mpaka jioni.
Who We AreWhat We EelieveWhat We Do
2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.