1Lile fujo lilipotulia, Paulo akatuma watu kuwaita wanafunzi, akawatuliza mioyo, akaagana nao, akaondoka kwenda Makedonia.
2Akapita pande zile akiwatuliza mioyo na kuwaambia maneno mengi, kisha akafidka Ugriki.
3Akakaa huko miezi mitatu. Alipotaka kuingia chomboni, aende Ushami, Wayuda walimlia njama. Kwa hiyo akapendezwa kurudi na kupita Makedonia.
4Waliofuatana naye mpaka Asia ni Sopatiro, mwana wa Puro wa Beroya, na Aristarko na Sekundo wa Tesalonike na Gayo wa Derbe na Timoteo; tena Tikiko na Tirofimo wa Asia.Paulo na wazee wa Efeso.
17*Lakini toka Mileto alituma mtu Efeso kuwaita wazee wa wateule.
18Hao walipofika kwake, akawaambia: Ninyi mnajua, nilivyokaa nanyi siku zote tangu siku ya kwanza, nilipofika Asia:
Who We AreWhat We EelieveWhat We Do
2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.