1Waisiraeli walipokaa Sitimu, watu wakaanza kufanya ugoni na wanawake wa Kimoabu.
2Nao walipowaalikia matambiko ya miungu yao, nao hao watu wakala nyama za tambiko, hata miungu yao wakaiangukia.
10Kisha Bwana akamwambia Mose kwamba:
11Pinehasi, mwana wa Elazari, mwana wa mtambikaji Haroni, ameyarudisha nyuma machafuko yangu makali, yawaondokee wana wa Isiraeli; kwani wivu, niliokuwa nao, uo huo ameuona naye katikati yao, kwa hiyo sikuwamaliza wana wa Isiraeli kwa wivu wangu.
12Kwa sababu hii umwambie: Vivi hivi ninamwekea agano la kumpatia utengemano.
16Kisha Bwana akamwambia Mose kwamba:
17Wainukieni Wamidiani, mwapige!4 Mose 31:2-10.
18Kwani ndio wanaowachukia ninyi kwa madanganyo yao walipowadanganya na matambiko ya Baali-Peori, tena wamewadanganya na kuwapa ndugu yao mke, yule Kozibi, binti mkuu wa Wamidiani, ni yule aliyeuawa siku hiyo, pigo lilipowapata kwa ajili ya Peori.
Who We AreWhat We EelieveWhat We Do
2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.