1Miriamu na Haroni wakamteta Mose kwa ajili ya mke wa Kinubi, aliyemwoa; kwani Mose alioa mwanamke wa Kinubi.
11Ndipo, Haroni alipomwambia Mose: E Bwana wangu, usitutwike hilo kosa letu, tulilolikosa kwa upumbavu!
12Huyu umbu letu asiwe kama mfu aliyekwisha kuliwa nusu ya nyama za mwili wake hapo, alipotoka tumboni mwa mama yake.
13Mose akamlilia Bwana kwamba: E Mungu, ninakuomba sana, umponye.2 Mose 15:26.
14Bwana akamwambia Mose: Kama baba yake angalimtemea mate usoni pake, hangaliona soni siku saba? Na afungiwe siku saba nje ya makambi, baadaye na arudishwe tena.3 Mose 13:46.
15Kwa hiyo Miriamu akafungiwa nje ya makambi siku saba, nao watu hawakuondoka kwenda safari yao, mpaka Miriamu akarudishwa.
16Kisha watu wakaondoka Haseroti kwenda safari yao, wakapiga makambi katika nyika ya Parani.
Who We AreWhat We EelieveWhat We Do
2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.