1Alipokuwa akitambea akaona amtu aliyekuwa kipofu tangu kuzaliwa.
8Majirani zake nao waliomwona siku zote, alivyokaa na kuombaomba, wakasema: Huyu siye aliyekuwa amekaa na kuombaomba?
9Wengine wakasema: Ndiye; wengine wakasema: Siye, wamefanana tu; yeye akasema: Mimi ndiye.
10Basi, wakamwuliza: Macho yako yamefumbukaje?
11Akajibu: Yule mtu anayeitwa Yesu alivuruga kitope, akanipaka machoni, akaniambia: Uende penye ziwa la Siloa, unawe! Nikaenda, nikanawa, nikapata kuona.
12Walipomwuliza: Yuko wapi huyo? akasema: Sijui.
13Wakampeleka kwa Mafariseo yule aliyekuwa ni kipofu.
14Lakini siku, Yesu alipokivuruga kitope na kumfumbua macho yake, ilikuwa ya mapumziko.
35Kisha Yesu akasikia, ya kuwa wamemfukuza, atoke; alipomwona akasema: Unamtegemea Mwana wa mtu?
36Yule akajibu, akasema: Ni yupi, Bwana, nipate kumtegemea?
37Yesu akamwambia: Umekwisha kumwona, naye anayesema na wewe ndiye.
Who We AreWhat We EelieveWhat We Do
2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.