Yohana 9 - Swahili Roehl Bible 1937

Mtu aliyekuwa kipofu tangu kuzaliwa.

1Alipokuwa akitambea akaona amtu aliyekuwa kipofu tangu kuzaliwa.

8Majirani zake nao waliomwona siku zote, alivyokaa na kuombaomba, wakasema: Huyu siye aliyekuwa amekaa na kuombaomba?

9Wengine wakasema: Ndiye; wengine wakasema: Siye, wamefanana tu; yeye akasema: Mimi ndiye.

10Basi, wakamwuliza: Macho yako yamefumbukaje?

11Akajibu: Yule mtu anayeitwa Yesu alivuruga kitope, akanipaka machoni, akaniambia: Uende penye ziwa la Siloa, unawe! Nikaenda, nikanawa, nikapata kuona.

12Walipomwuliza: Yuko wapi huyo? akasema: Sijui.

13Wakampeleka kwa Mafariseo yule aliyekuwa ni kipofu.

14Lakini siku, Yesu alipokivuruga kitope na kumfumbua macho yake, ilikuwa ya mapumziko.

35Kisha Yesu akasikia, ya kuwa wamemfukuza, atoke; alipomwona akasema: Unamtegemea Mwana wa mtu?

36Yule akajibu, akasema: Ni yupi, Bwana, nipate kumtegemea?

37Yesu akamwambia: Umekwisha kumwona, naye anayesema na wewe ndiye.

Blog
About Us
Message
Site Map

Who We AreWhat We EelieveWhat We Do

Terms of UsePrivacy Notice

2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.

Home
Gospel
Question
Blog
Help