Yohana 18 - Swahili Roehl Bible 1937

Kuchongewa na Yuda.

1Yesu alipokwisha kuyasema haya akatoka pamoja na wanafunzi wake kwenda ng'ambo ya kijito cha Kidoroni, kulikokuwa na kiunga. Humo wakaingia yeye na wanafunzi wake.(2-11: Mat. 26:47-56; Mar. 14:43-52; Luk. 22:47-53.)

2Lakini naye Yuda aliyemchongea alipajua hapo, kwani Yesu na wanafunzi wake walikusanyika mara nyingi hapo.Kukana kwa Petero.(12-27: Mat. 26:57-75; Mar. 14:53-72; Luk. 22:54-71.)

12Kisha kikosi cha askari na mkubwa wao na watumishi wa Wayuda wakamkamata Yesu, wakamfunga.

13Wakampeleka kwanza kwa Ana; kwani alikuwa mkwewe Kayafa aliyekuwa mtambikaji mkuu wa mwaka ule.

14Kayafa ndiye yule aliyekula njama na Wayuda kwamba: Inafaa, mtu mmoja afe kwa ajili ya watu.

33Pilato akaingia tena bomani, akamwita Yesu, akamwuliza: Wewe ndiwe mfalme wa Wayuda?

34Yesu akajibu: Wasema hivi kwa mawazo yako mwenyewe, au wako wengine waliokusimulia mambo yangu?

35Pilato akajibu: Je? Mimi Myuda? Wao wa taifa lako na watambikaji wakuu wamekuleta kwangu. Umefanya nini?

36Yesu akajibu: Ufalme wangu sio wa ulimwengu huu. Kama ufalme wangu ungekuwa wa ulimwengu huu, watumishi wangu wangeupigania, nisitiwe mikononi mwa Wayuda. Lakini sasa ufalme wangu sio wa hapa.

37Pilato akamwuliza: Basi, wewe u mfalme gani? Yesu akajibu: Wewe unavyosema, ndivyo: mimi ni mfalme. Niliyozaliwa, tena niliyojia ulimwenguni, ndiyo hii: niishuhudie iliyo ya kweli! Kila aliye na kweli huisikia sauti yangu.1 Tim. 6:13.

38Pilato akamwambia: Iliyo ya kweli ndiyo nini? Alipokwisha kuyasema haya akawatokea tena Wayuda, akawaambia: Mimi sioni kwake neno la kumhukumu.

39Lakini iko desturi kwenu, niwafungulie mmoja siku ya Pasaka; basi, mwataka, niwafungulie mfalme wa Wayuda?

40Ndipo, walipopiga makelele tena wakisema: Huyu hatumtaki, twamtaka Baraba; naye Baraba alikuwa mnyang'anyi.

Blog
About Us
Message
Site Map

Who We AreWhat We EelieveWhat We Do

Terms of UsePrivacy Notice

2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.

Home
Gospel
Question
Blog
Help