1Bwana akamkagua Sara, kama alivyosema; naye Bwana akamfanyizia Sara, kama alivyomwagia.
14Kesho yake Aburahamu akaamka na mapema, akachukua mkate na kibuyu cha maji, akampagaza Hagari begani, kisha akampa na mwanawe; ndivyo, alivyompa ruhusa kwenda zake. Lakini alipokwenda akapotea katika nyika ya Beri-Seba.
15Maji yalipokwisha kibuyuni, akamwacha mwanawe chini ya kijiti,
16akaenda kukaa peke yake na kumwelekea mbali kidogo kama hapo, mtu anapotupa mshale kwa upindi, kwani alisema: Nisione, mwana anavyokufa! Alipokaa hivyo na kumwelekea akapaza sauti yake, akalia.
17Mungu alipokisikia kilio cha mtoto, malaika wa Mungu akamwita Hagari toka mbinguni, akamwambia: Una nini, Hagari? Usiogope! Kwani Mungu amekisikia kilio cha mtoto hapo, anapolala.
18Inuka, umwinue mtoto na kumshika kwa mkono wako! Kwani nitamfanya kuwa taifa kubwa.
19Kisha Mungu akamfumbua macho; ndipo, alipoona kisima cha maji, akaenda kukijaza kile kibuyu, akampa mtoto, anywe.
20Mungu akawa na huyu mtoto, akakua, akakaa nyikani, akawa mpiga upindi.
21Akakaa katika nyika ya Parani; naye mama yake akamwoza mwanamke wa nchi ya Misri.Maagano ya Aburahamu na Abimeleki.
22Ikawa wakati huo, ndipo, Abimeleki na Pikoli, mkuu wa vikosi vyake, walipomwambia Aburahamu kwamba: Mungu yuko pamoja na wewe katika mambo yote, unayoyafanya.1 Mose 26:26.
23Sasa niapie na kumtaja Mungu kwamba: Hutanidanganya mimi wala wao wa uzao wangu wajao nyuma yangu, ila huo wema, niliokufanyia wewe, unifanyie mimi nayo nchi hii, unayoikaa ugeni!1 Mose 20:15.
24Aburahamu akasema: Basi, mimi nitaapa.
25Kisha Aburahamu akamwonya Abimeleki kwa ajili ya kisima cha maji, watumishi wake Abimeleki walichokinyang'anya.1 Mose 26:15,18.
26Naye Abimeleki akasema: Simjui aliyelifanya jambo hilo, wewe nawe hujanipasha habari, mimi nami sijavisikia, ni leo hivi tu.
27Kisha Aburahamu akachukua mbuzi na kondoo na ng'ombe, akampa Abimeleki; hivyo ndivyo, wao wawili walivyofanya agano.
28Aburahamu akaweka wana kondoo saba peke yao,
29naye Abimeleki akamwuliza Aburahamu: Hawa wana kondoo saba ukiwaweka peke yao, ni wa nini?
30Akajibu: Hawa wana kondoo saba wa kike wachukue mkononi mwangu, upate kunishuhudia, ya kuwa nilikichimbua kisima hiki.
31Kwa sababu hii wakapaita mahali pale Beri-Seba (Kisima cha Kiapo), kwa kuwa waliapiana hapo wote wawili.1 Mose 26:33.
32Walipokwisha kulifanya agano hilo hapo Beri-Seba, Abimeleki na Pikoli, mkuu wa vikosi vyake, wakaondoka, wakarudi katika nchi ya Wafilisti.
33Aburahamu akapanda mvinje hapo Beri-Seba, akalitambikia hapo Jina la Bwana aliye Mungu wa kale na kale.1 Mose 12:8; Yes. 40:28; Rom. 16:26.
34Aburahamu akakaa ugenini katika nchi ya Wafilisti siku nyingi.
Who We AreWhat We EelieveWhat We Do
2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.