Ezekieli 37 - Swahili Roehl Bible 1937

Ufufuko wa Waisiraeli.

1Mkono wa Bwana ukanishika, Bwana akanitoa kirohoroho, akanipeleka na kuniweka katikati ya hilo bonde, nalo lilikuwa limejaa mifupa.

2Akanipitisha po pote pande zote, ilipokuwa, nikaiona kuwa mingi sana humo bondeni juu ya mchanga, nami nikaiona kuwa mikavu sana.

3Akaniuliza: Mwana wa mtu, inakuwaje? Mifupa hii itaweza kuwa yenye uzima tena? Nikajibu: Bwana Mungu wewe unajua.

4Akaniambia: Ifumbulie mifupa hii yatakayokuwa! Iambie: Ninyi mifupa mikavu, sikieni neno la Bwana!

5Hivi ndivyo, Bwana Mungu anavyoiambia mifupa hii: Tazameni, nitawaletea pumzi ndani yenu, mpate kuwa wenye uzima tena.

Blog
About Us
Message
Site Map

Who We AreWhat We EelieveWhat We Do

Terms of UsePrivacy Notice

2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.

Home
Gospel
Question
Blog
Help