1Isiraeli akaondoka pamoja nayo yote, aliyokuwa nayo, akaja Beri-Seba; ndiko, alikomchinjia Mungu wa baba yake Isaka ng'ombe za tambiko.Yosefu anampokea baba yake Yakobo.
28Yakobo akamtuma Yuda kwenda mbele yake kwa Yosefu, amwonyeshe nchi ya Goseni, kisha wakaiingia hiyo nchi ya Goseni.
31Kisha Yosefu akawaambia ndugu zake nao wa mlango wa baba yake: Nitapanda kumpasha Farao habari ya kwamba: Ndugu zangu nao wa mlango wa baba yangu waliokaa katika nchi ya Kanaani wamefika kwangu.
32Nao watu hawa ni wachungaji, kwani ni wenye makundi, nao mbuzi na kondoo wao na ng'ombe wao nayo yote, waliyokuwa nayo, wameyaleta huku.
33Naye Farao atakapowaita na kuwauliza: Kazi yenu nini?
34na mmwambie: Watumwa wako ni wachungaji tangu ujana wetu mpaka sasa; nasi tulivyo, ndivyo, nao baba zetu walivyokuwa, kusudi mpate kukaa katika nchi ya Goseni; kwani Wamisri huwachukiza wachungaji wote.
Who We AreWhat We EelieveWhat We Do
2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.