1Bwana akamwambia Mose kwamba:
2Waagize wana wa Isiraeli, wakupatie mafuta ya chekele yaliyotwangwa vema kuwa safi ya kinara ya kutia siku zote katika taa zake.Mapatilizo yao wanaoumiza wenzao.
17Mtu akimpiga mwenzake, afe, sharti auawe naye.
18Lakini akipiga nyama, naye akifa, sharti amlipe, nyama aliye mzima kwa yule aliyekufa.2 Mose 21:12.
19Mtu akimwumiza mwenziwe, apate kilema, naye sharti afanyiziwe yaleyale, aliyoyafanya:2 Mose 21:23-25.
20kidonda kwa kidonda, jicho kwa jicho, jino kwa jino. Kilema, alichompatia mwenzake, apatiwe naye.
21Ni hivi: mtu atakayempiga nyama, naye akifa, sharti amlipe; lakini mtu atakayempiga mwenziwe, naye akifa, sharti auawe.
22Hukumu za kwenu sharti ziwe moja, mwenye kuhukumiwa kama ni mgeni au kama ni mwenyeji. Kwani mimi Bwana ni Mungu wenu.2 Mose 12:49; 3 Mose 19:34.
23Mose alipokwisha kuwaambia wana wa Isiraeli maneno haya, wakamtokeza yule mwenye kutukana nje ya makambi, wakamwua kwa kumpiga mawe; wana wa Isiraeli wakafanya, kama Bwana alivyomwagiza Mose.
Who We AreWhat We EelieveWhat We Do
2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.