Mashangilio 12 - Swahili Roehl Bible 1937

Wamchao Mungu hutulia, ijapo wasingiziwe.Kwa mwimbishaji, wa kuimba zeze lenye nyuzi nane. Wimbo wa Dawidi.

1Okoa, Bwana! Kwani wamekwisha wao wakuchao, nao wakutegemeao wametoweka kwenye wana wa watu.

2Kila mtu na mwenzake husemeana yaliyo uwongo, midomo yao husema yenye ujanja, kwa kuwa wenye mioyo miwili.

3Bwana na akomeshe midomo yote yaliyo yenye ujanja, nazo ndimi zisemazo maneno makuu tu!

4Ndio wanaosema: kwa nguvu za ndimi zetu tutashinda sisi, nayo mikono yetu hutusaidia; yuko nani atakayetutawala?

5Kwa ajili ya taabu zao walio wanyonge na kwa ajili ya yowe zao walio wakiwa nitainuka sasa, ndivyo, Bwana asemavyo, niwapatie wokovu wauchuchumiao.

6Maneno ya Bwana ndiyo maneno yaliyo mang'avu hufanana na fedha zilizoyeyushwa chunguni huku nchini, zilizong'azwa hivyo mara saba.

Blog
About Us
Message
Site Map

Who We AreWhat We EelieveWhat We Do

Terms of UsePrivacy Notice

2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.

Home
Gospel
Question
Blog
Help