1Hayo yalipokwisha kufanyika, kulikuwa na mtu wa Izireeli, ndiye Naboti; alikuwa na shamba la mizabibu huko Izireeli karibu ya jumba la Ahabu, mfalme wa Samaria.
2Ahabu akamwambia Naboti: Nipe shamba lako la mizabibu, liwe langu, nipapande mboga! Kwani ni karibu ya nyumba yangu. Nami mahali pake nitakupa shamba la mizabibu lililo zuri zaidi, au kama unapendezwa, nitakupa fedha kuwa malipo yake.
3Naboti akamwambia Ahabu: Bwana na anizuie, nisikupe fungu langu, nililolipata kwa baba zangu!
4Ahabu akaenda nyumbani mwake mwenye moyo uliokasirika na kuchafuka kwa ajili ya hilo neno, Naboti wa Izireeli alilomwambia kwamba: Sitakupa fungu langu, nililolipata kwa baba zangu. Akaja kulala kitandani pake, akauelekeza uso ukutani, akakataa kula chakula.
5Ndipo, mkewe Izebeli alipoingia mwake, akamwambia: Mbona roho yako inakasirika, ukakataa kula?
6Akamwambia: Nimesema na Naboti wa Izireeli, nikamwambia: Nipe shamba lako la mizabibu kwa fedha, au kama unapendezwa, nitakupa shamba jingine la mizabibu mahali pake; naye akajibu: Sitakupa shamba langu la mizabibu.
7Mkewe Izebeli akamwambia: Sasa wewe sharti uonyeshe, ya kuwa ndiwe mfalme wa Waisiraeli; inuka, ule, nao moyo wako na utulie! Mimi nitakupa shamba la mizabibu la Naboti wa Izireeli.
8Akaandika barua katika jina la Ahabu, akaitia muhuri ya mfalme, akaituma hiyo barua kwa wazee na kwa wakuu wa mji waliokaa humo na Naboti.
9Akaandika humo baruani kwamba: Tangazeni mfungo, naye Naboti mwekeni kuwa mkuu wa watu!
10Kisha wekeni kila kando yake watu wawili wasiofaa, wapate kumsingizia kwamba: Amemtukana Mungu na mfalme. Kisha mtoeni mjini, mmpige mawe, afe!
Who We AreWhat We EelieveWhat We Do
2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.