Mashangilio 9 - Swahili Roehl Bible 1937

Kuomba msaada wa Mungu apatilizaye wachukivu wasiomcha.Kwa mwimbishaji, wa kuimba kama wimbo: Mfie mwanao! Wimbo wa Dawidi.

1Nitamshukuru Bwana kwa moyo wangu wote, nitayasimulia mataajabu yako, uliyoyafanya yote.

2Kwa kufurahi nitakushangilia, nitaliimbia Jina lako wewe ulioko huko juu,

3kwani adui zangu wamerudi nyuma, wakajikwaa, wakaangamia machoni pako.

4Maana umenipatia kushinda, nilipohukumiwa, ukakalia kiti cha uamuzi, utoe hukumu iongokayo.

7Bwana hukaa kale na kale, akakisimika kiti chake, atoe hukumu.

15Wamizimu wamedidimia katika shimo, walilolifanya wao, miguu yao ikanaswa katika tanzi, walilolitega wenyewe.

19Inuka, Bwana, watu wasikaze nguvu, wamizimu wahukumiwe machoni pako!

20Wakemee wamizimu, Bwana, kusudi wastushwe, kusudi wajitambue kuwa watu tu!

Blog
About Us
Message
Site Map

Who We AreWhat We EelieveWhat We Do

Terms of UsePrivacy Notice

2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.

Home
Gospel
Question
Blog
Help