Mifano 4 - Swahili Roehl Bible 1937

Vijana sharti wafuate mafundisho yenye ujuzi.

1Wanangu, sikieni, baba akiwakanya!

Yategeni masikio, myajue yenye utambuzi!

2Kwani ninawapa ninyi mafundisho mema:

maonyo yangu msiyaache!

3Kwani nami nilipokuwa mwana wa baba yangu,

mtoto mnyonge aliyependwa sana na mama kwa kuwa wa pekee,

4baba alinifundisha, akaniambia:

Moyo wako sharti uyashike sana maneno yangu,

uyaangalie maagizo yangu! Ndipo, utakapopata uzima.

10Sikia, mwanangu, uyapokee maneno yangu!

Ndipo, miaka yako ya kukaa uzimani itakapokuwa mingi.

20Mwanangu, yasikilize maneno yangu

Yategee sikio, ninayokuambia!

21Usiyaache, yatoweke machoni pako!

Yaangalie moyoni mwako ndani!

22Kwani hayo ndio uzima wao wayapatao,

tena ni dawa ya miili yao wote.

Blog
About Us
Message
Site Map

Who We AreWhat We EelieveWhat We Do

Terms of UsePrivacy Notice

2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.

Home
Gospel
Question
Blog
Help