1*Siku zilezile walikuwapo watu waliomsimulia ya Wagalilea, ambao Pilato alimwaga damu zao na kuzichanganya na damu za ng'ombe zao za tambiko.
2Akajibu akiwaambia: Mwadhani, Wagalilea hao walikuwa wakosaji kuwapita Wagalilea wote, maana wameteswa hivyo?Kuulilia mji wa Yerusalemu.
31Saa ileile wakawako Mafariseo waliomjia, wakamwambia: Toka hapa, ujiendee! kwani Herode anataka kukuua.
32Akawaambia: Nendeni, mkamwambie mbweha huyo: Tazama, leo na kesho nafukuza pepo na kuponya wagonjwa, nayo siku ya tatu mambo yangu yatamalizika.
33Lakini leo na kesho na kesho kutwa sharti niende, kwani haiwezekani, mfumbuaji auawe, isipokuwa Yerusalemu.
(34-35: Mat. 23:37-39.)34Yerusalemu, Yerusalemu, unawaua wafumbuaji, ukawapiga mawe waliotumwa kwako! Mara ngapi nimetaka kuwakusanya watoto wako, kama kuku anavyovikusanya vifaranga vyake mabawani! Lakini hamkutaka!
35Mtaona, Nyumba yenu ikiachwa, iwe peke yake! Nawaambiani: Hamtaniona tena mpaka siku ile, mtakaposema: Na atukuzwe ajaye kwa Jina la Bwana!
Who We AreWhat We EelieveWhat We Do
2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.