3Yohana UTANGULIZI - Bible in Kiswahili, Revised Union Version 2013

UTANGULIZIWaraka huu umeandikwa na Yohana ambaye anajiita “Mzee” (tazama utangulizi kwa Waraka wa Kwanza wa Yohana). Ijapokuwa Waraka huu unawekwa kwenye kundi la “Nyaraka kwa Watu Wote” inaonekana kwamba ulitumwa kwa mtu binafsi aitwaye Gayo ambaye alikuwa rafiki yake mwandishi.Katika kanisa fulani huko Asia Ndogo alikuwapo kiongozi aliyependa kuchukua madaraka. Huyo anaitwa Diotrefe. Diotrefe alikataa kupokea waalimu na wahubiri halali waliofundisha ukweli wa Injili. Vile vile hakutaka kupokea wajumbe waliotoka kwa mtume Yohana na hivyo kumkataa Mtume Yohana mwenyewe.Waraka unamtia moyo Gayo aliyekuwa mmoja wa viongozi katika kanisa hilo apokee na kusaidia Wakristo waliosafiri wakihubiri na kufundisha ukweli wa Injili. Anamtahadharisha Gayo kuhusu Diotrefe na kumsifu Demetrio na wengine wanaowapa msaada wahubiri wa kweli.
Blog
About Us
Message
Site Map

Who We AreWhat We EelieveWhat We Do

Terms of UsePrivacy Notice

2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.

Home
Gospel
Question
Blog
Help