1 Wathesalonike 4 - Bible in Kiswahili, Revised Union Version 2013

Maisha yampendezayo Mungu

1 2 The 3:6 Iliyobaki, ndugu, tunawasihi na kuwaonya kwamba mwenende katika Bwana Yesu; kama mlivyopokea kwetu jinsi iwapasavyo kuenenda na kumpendeza Mungu, kama nanyi mnavyoenenda, vivyo hivyo mpate kuzidi sana.

2Kwa kuwa mnajua ni maagizo gani tuliyowapa kwa Bwana Yesu.

31 The 5:23; Ebr 10:10; 1 Pet 1:16 Maana haya ndiyo mapenzi ya Mungu, kutakaswa kwenu, mwepukane na uasherati;

41 Kor 6:13,15 kila mmoja wenu ajue kuuweza mwili wake katika utakatifu na heshima;

5Yer 10:25; Zab 79:6 si katika hali ya tamaa mbaya, kama Mataifa wasiomjua Mungu.

6Zab 94:2 Mtu asimpunje ndugu yake wala kumkosea katika jambo hili; kwa sababu Bwana ndiye alipizaye kisasi cha haya yote; kama tulivyowaambia kwanza, tukashuhudia sana.

72 The 2:13,14 Maana Mungu hakutuitia uchafu, bali tuwe katika utakaso.

8Lk 10:16; Eze 36:27; 37:14 Basi yeye anayekataa, hakatai mwanadamu bali Mungu, anayewapa ninyi Roho wake Mtakatifu.

9 Yn 13:34; Yer 31:33,34 Kuhusu upendano, hamna haja niwaandikie; maana ninyi wenyewe mmefundishwa na Mungu kupendana.

102 The 3:4 Kwa maana mnafanya neno hili kwa ndugu wote walio katika Makedonia yote. Lakini tunawasihi, ndugu, mzidi sana.

11Efe 4:28; 2 The 3:8,12 Tena mjitahidi kutulia, na kutenda shughuli zenu, na kufanya kazi kwa mikono yenu wenyewe, kama tulivyowaagiza;

12Kol 4:5; 1 Kor 5:12,13 ili mwende kwa adabu mbele yao walio nje, wala msiwe na haja ya kitu chochote.

Kuja kwa Bwana

13 1 Kor 15:20; Efe 2:12 Lakini, ndugu, hatutaki msijue habari zao waliolala mauti, msije mkahuzunika kama na wengine wasio na matumaini.

14Rum 14:9; 1 Kor 15:3,4,12 Maana, ikiwa tunaamini ya kwamba Yesu alikufa akafufuka, vivyo hivyo na hao waliolala katika Yesu, Mungu atawaleta pamoja naye.

151 Kor 15:51-52; 7:10,25 Kwa kuwa tunawaambieni haya kwa neno la Bwana, kwamba sisi tulio hai, tutakaosalia hata wakati wa kuja kwake Bwana, hakika hatutawatangulia wao waliokwisha kulala mauti.

161 Kor 15:52; 2 The 1:7 Kwa sababu Bwana mwenyewe atashuka kutoka mbinguni pamoja na mwaliko, na sauti ya malaika mkuu, na parapanda ya Mungu; nao waliokufa katika Kristo watafufuliwa kwanza.

17Yn 12:26; 17:24 Kisha sisi tulio hai, tuliosalia, tutanyakuliwa pamoja nao katika mawingu, ili tumlaki Bwana hewani; na hivyo tutakuwa pamoja na Bwana milele.

18Basi, farijianeni kwa maneno hayo.

Blog
About Us
Message
Site Map

Who We AreWhat We EelieveWhat We Do

Terms of UsePrivacy Notice

2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.

Home
Gospel
Question
Blog
Help