1
40 Mwa 25:23; 36:8; 2 Fal 8:20; 2 Sam 8:14; Oba 1:18-20 Kwa upanga wako wewe utaishi, nawe utamtumikia nduguyo;
Na itakuwa utakapoponyoka,
Utalivunja kongwa lake katika shingo yako.
Yakobo akwepa ghadhabu ya Esau41 Mwa 37:4; 50:3; Oba 1:10; 1 Yoh 3:12 Esau akamchukia Yakobo kwa ajili ya ile baraka babaye aliyombariki. Esau akasema moyoni mwake, Siku za kumlilia baba yangu zinakaribia, ndipo nitakapomwua ndugu yangu Yakobo.
42Zab 64:5 Rebeka akaarifiwa maneno ya Esau, mwanawe mkubwa. Akatuma mtu kumwita Yakobo, mwanawe mdogo, akamwambia, Tazama, katika habari zake Esau, ndugu yako, anajifariji moyo wake, maana anakusudia kukuua.
43Mwa 11:31 Na sasa, mwanangu, sikia sauti yangu, uondoke, ukimbilie kwa Labani, ndugu yangu huko Harani;
44ukae kwake siku chache, hadi ghadhabu ya ndugu yako iishe;
45hadi ikuondokee ghadhabu ya ndugu yako, akasahau uliyomtenda. Ndipo nitakapotuma watu kukuchukua kutoka huko. Kwa nini nifiwe nanyi nyote wawili siku moja?
46 Mwa 24:3; 26:35; 28:8 Rebeka akamwambia Isaka, Rohoni mwangu sina raha kwa sababu ya hao binti za Hethi. Kama Yakobo akitwaa mke katika binti za Hethi, kama hawa binti za nchi, maisha yangu yatanifaidi nini?
Who We AreWhat We EelieveWhat We Do
2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.