Zaburi 98 - Bible in Kiswahili, Revised Union Version 2013

Sifa kwa mwamuzi wa DuniaZaburi.

1 Isa 59:16 Mwimbieni BWANA wimbo mpya,

Kwa maana ametenda mambo ya ajabu.

Mkono wa kulia,

Na mkono wake mtakatifu umemtendea wokovu.

2 Isa 52:10; Lk 2:30; Isa 62:2; Rum 3:25; Kum 4:31; Mik 7:20; Lk 1:54; Isa 49:6; Lk 3:6; Mdo 13:47 BWANA ameufunua wokovu wake,

Machoni pa mataifa ameidhihirisha haki yake.

3Amezikumbuka rehema zake,

Na uaminifu wake kwa nyumba ya Israeli.

Miisho yote ya dunia imeuona

Wokovu wa Mungu wetu.

4Mshangilieni BWANA, nchi yote,

Inueni sauti, imbeni kwa furaha, imbeni sifa.

5Mwimbieni BWANA sifa kwa kinubi,

Kwa kinubi na sauti tamu.

6 Hes 10:10; 1 Nya 15:28; 2 Nya 29:27 Kwa panda na sauti ya baragumu.

Shangilieni mbele za Mfalme, BWANA.

7Bahari na ivume na vyote viijazavyo,

Ulimwengu nao wanaokaa ndani yake.

8Mito na ipige makofi,

Milima na iimbe pamoja kwa furaha.

9Mbele za BWANA;

Kwa maana anakuja kuihukumu nchi.

Atauhukumu ulimwengu kwa uaminifu,

Na mataifa kwa adili.

Blog
About Us
Message
Site Map

Who We AreWhat We EelieveWhat We Do

Terms of UsePrivacy Notice

2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.

Home
Gospel
Question
Blog
Help