Ayubu 27 - Bible in Kiswahili, Revised Union Version 2013

Ayubu ashikilia uelekevu wake

1Kisha Ayubu akaendelea na hoja yake, na kusema,

2 Ayu 34:5 Kama aishivyo Mungu, aliyeniondolea haki yangu;

Huyo Mwenyezi aliyeitesa nafsi yangu;

3(Kwa kuwa uhai wangu ungali mzima ndani yangu,

Na Roho ya Mungu iko katika pua yangu;)

4Hakika midomo yangu haitanena yasiyo haki,

Wala ulimi wangu hautatamka udanganyifu.

5 Ayu 13:15 Hasha! Nisiwahesabie ninyi kuwa na haki;

Hata nitakapokufa sitajiondolea uelekevu wangu.

6 Ayu 2:3; Mdo 24:16 Haki yangu naishika sana, wala sitaiacha;

Moyo wangu hautanisuta wakati nikiwapo hai.

7Adui yangu na awe kama huyo mwovu,

Na mpinzani wangu awe kama asiye haki.

8 Mt 16:26 Maana tumaini la mpotovu ni nini, ingawa ajipatia faida,

Hapo Mungu amwondoleapo roho yake?

9 Mit 1:28; Isa 1:15; Mik 3:4; Zek 7:13; Yak 4:3 Je! Mungu atakisikia kilio chake,

Taabu zitakapomfikia?

10 Ayu 22:26 Je! Atajifurahisha katika Mwenyezi,

Na kumlingana Mungu nyakati zote?

11Nitawafundisha ninyi mambo ya mkono wa Mungu;

Hayo yaliyo kwa Mwenyezi sitayaficha.

12Tazama, ninyi nyote mmeyaona wenyewe;

Mbona basi mmebatilika kabisa?

13Hii ndiyo sehemu ya mtu mwovu kwa Mungu,

Na urithi wa hao waoneao, waupokeao kwa Mwenyezi.

14 Kum 28:32,41; Est 9:10; 2 Fal 10:6-10 Watoto wake wakiongezeka ni kwa upanga;

Na wazao wake hawatashiba chakula.

15 Zab 78:64 Hao watakaosalia kwake watakufa kwa maradhi mabaya,

Wala wajane wake waliofiwa na waume hawataomboleza.

16Ajapokusanya fedha kama mavumbi,

Na kujifanyia mavazi kama udongo kwa wingi;

17 Mit 28:8; Mhu 2:26 Yamkini kuyatengeza, lakini wenye haki watayavaa,

Nao wasio na hatia watazigawanya hizo fedha.

18 Omb 2:6 Yeye hujenga nyumba yake kama mdudu,

Na kama kibanda afanyacho mlinzi.

19 Hes 20:26 Yeye hujilaza hali ni tajiri, lakini ndio mwisho;

Hufunua macho yake, naye hayuko.

20Vitisho vyampata kama maji mengi;

Dhoruba humwiba usiku.

21Upepo wa mashariki humchukua, naye huondoka;

Na kumkumba atoke mahali pake.

22Kwani Mungu atamtupia asimhurumie;

Angependa kuukimbia mkono wake.

23Watu watampigia makofi,

Na kumzomea atoke mahali pake.

Blog
About Us
Message
Site Map

Who We AreWhat We EelieveWhat We Do

Terms of UsePrivacy Notice

2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.

Home
Gospel
Question
Blog
Help