Isaya 12 - Bible in Kiswahili, Revised Union Version 2013

Shukrani na sifa

1 Isa 2:11; Zek 14:20,21 Na katika siku hiyo utasema,

Ee BWANA, nitakushukuru wewe;

Kwa kuwa ijapokuwa ulinikasirikia,

Hasira yako imegeukia mbali,

Nawe unanifariji moyo.

2 Kut 15:2; Zab 118:14 Tazama, Mungu ndiye wokovu wangu;

Nitatumaini wala sitaogopa;

Maana BWANA YEHOVA ni nguvu zangu na wimbo wangu;

Naye amekuwa wokovu wangu.

3 Yer 2:13; Yn 4:10,14 Basi, kwa furaha mtateka maji katika visima vya wokovu.

4Na katika siku hiyo mtasema,

Mshukuruni BWANA, liitieni jina lake;

Yatangazeni matendo yake kati ya mataifa,

Litangazeni jina lake kuwa limetukuka.

5Mwimbieni BWANA; kwa kuwa ametenda makuu;

Na yajulikane haya katika dunia yote.

6 Isa 54:1; Sef 3:14; Lk 19:37-40 Paza sauti, piga kelele, mwenyeji wa Sayuni;

Maana Mtakatifu wa Israeli ni mkuu kati yako.

Blog
About Us
Message
Site Map

Who We AreWhat We EelieveWhat We Do

Terms of UsePrivacy Notice

2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.

Home
Gospel
Question
Blog
Help