1Katika shida yangu nilimlilia BWANA
Naye akaniitikia.
2Ee BWANA, uniponye
Na midomo ya uongo na ulimi wa hila.
3Akupe nini, akuzidishie nini,
Ewe ulimi wenye hila?
4Mishale ya mtu hodari iliyochongoka,
Pamoja na makaa ya mretemu.
5 Mwa 10:2; 1 Sam 25:1; Yer 49:28 Ole wangu mimi!
Kwa kuwa ni mgeni katika Mesheki;
Na kufanya makao yangu
Katikati ya hema za Kedari.
6Kwa muda mrefu nimeishi,
Pamoja na watu wanaoichukia amani.
7Mimi nazingatia amani;
Bali ninenapo, wao wanataka vita.
Who We AreWhat We EelieveWhat We Do
2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.