Zaburi 120 - Bible in Kiswahili, Revised Union Version 2013

Sala ya ukomboziWimbo wa Kupanda mlima.

1Katika shida yangu nilimlilia BWANA

Naye akaniitikia.

2Ee BWANA, uniponye

Na midomo ya uongo na ulimi wa hila.

3Akupe nini, akuzidishie nini,

Ewe ulimi wenye hila?

4Mishale ya mtu hodari iliyochongoka,

Pamoja na makaa ya mretemu.

5 Mwa 10:2; 1 Sam 25:1; Yer 49:28 Ole wangu mimi!

Kwa kuwa ni mgeni katika Mesheki;

Na kufanya makao yangu

Katikati ya hema za Kedari.

6Kwa muda mrefu nimeishi,

Pamoja na watu wanaoichukia amani.

7Mimi nazingatia amani;

Bali ninenapo, wao wanataka vita.

Blog
About Us
Message
Site Map

Who We AreWhat We EelieveWhat We Do

Terms of UsePrivacy Notice

2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.

Home
Gospel
Question
Blog
Help