1 1 Sam 22:1; 24:3 Kwa sauti yangu nitamlilia BWANA,
Kwa sauti yangu nitamwomba BWANA dua.
2Nitafunua mbele zake malalamiko yangu,
Shida yangu nitaitangaza mbele zake.
3Roho yangu inapozimia unayajua mapito yangu;
Katika njia niendayo wamenifichia mtego.
4Utazame mkono wangu wa kuume ukaone,
Kwa maana sina mtu anijuaye.
Makimbilio yamenipotea,
Hakuna wa kunitunza roho.
5 Omb 3:24 BWANA, nimekuita nikasema, Ndiwe kimbilio langu,
Fungu langu katika nchi ya walio hai.
6 Zab 116:6; 7:1 Ukisikilize kilio changu,
Kwa maana nimedhilika sana.
Uniponye kutoka kwao wanaonifuatia,
Kwa maana wao ni hodari kuliko mimi.
7 Zab 34:2; 119:17 Uitoe nafsi yangu kifungoni.
Nipate kulishukuru jina lako.
Wenye haki watanizunguka,
Kwa kuwa Wewe unanikirimu.
Who We AreWhat We EelieveWhat We Do
2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.