1Ee BWANA, nitakutukuza kwa maana umeniinua,
Wala hukuwafurahisha adui zangu juu yangu.
2 Zab 6:2-4 Ee BWANA, Mungu wangu,
Nilikulilia ukaniponya.
3 Zab 40:1,2 Umeniinua nafsi yangu,
Ee BWANA, kutoka kuzimu.
Umenihuisha na kunitoa
Miongoni mwao washukao Shimoni.
4Mwimbieni BWANA zaburi,
Enyi watauwa wake.
Na kutoa shukrani.
Kwa kukumbuka utakatifu wake.
5 Zab 16:11; Ufu 22:17 Maana ghadhabu zake ni za muda mfupi tu;
Radhi yake ni ya milele.
Kilio huweza kuwapo usiku,
Lakini furaha huja asubuhi.
6 Ayu 29:18 Nami nilipofanikiwa nilisema,
Sitaondoshwa milele.
7 Zab 104:29 BWANA, kwa radhi yako
Wewe uliuimarisha mlima wangu.
Uliuficha uso wako,
Nami nikafadhaika.
8Ee BWANA, nilikulilia Wewe,
Naam, kwa BWANA niliomba dua.
9 Zab 115:17 Mna faida gani katika damu yangu
Nishukapo Shimoni?
Mavumbi yatakusifu?
Yatautangaza uaminifu wako?
10 Zab 4:1 Ee BWANA, usikie, unirehemu,
BWANA, uwe msaidizi wangu.
11 2 Sam 6:14 Umegeuza msiba wangu kuwa ngoma;
Umeniondolea huzuni yangu, kunijalia furaha tele.
12Ili nafsi yangu ikusifu,
Wala isinyamaze.
Ee BWANA, Mungu wangu,
Nitakushukuru milele.
Who We AreWhat We EelieveWhat We Do
2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.