1 Eze 1:1; Dan 8:2; Isa 24:8; Omb 5:15; Amo 8:10; Ufu 18:22 Kando ya mito ya Babeli ndiko tulikoketi,
Tukalia tulipoikumbuka Sayuni.
2Katika miti iliyo katikati yake
Tulivitundika vinubi vyetu.
3Maana huko waliotuchukua mateka
Walitaka tuwaimbie;
Na waliotuonea walitaka tuwatumbuize;
Tuimbieni baadhi ya nyimbo za Sayuni.
4Twawezaje kuimba wimbo wa BWANA
Katika nchi ya ugeni?
5Nikikusahau, Ee Yerusalemu,
Mkono wangu wa kuume na upooze.
6 Eze 3:26 Ulimi wangu na ugandamane
Na kaakaa la kinywa changu, nisipokukumbuka.
Nisipoikuza Yerusalemu
Zaidi ya furaha yangu iliyo kuu.
7 Omb 4:22; Oba 1:10 Ee BWANA, uwakumbuke wana wa Edomu,
Siku ile Yerusalemu ilipotekwa.
Kwa namna walivyosema, Bomoeni!
Bomoeni hata misingini!
8 Isa 13:1; Ufu 18:6 Ee binti Babeli, uliye karibu na kuangamia,
Heri atakayekupatiliza, ulivyotupatiliza sisi.
9Heri yeye atakayewakamata wadogo wako,
Na kuwaseta wao juu ya mwamba.
Who We AreWhat We EelieveWhat We Do
2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.