Zaburi 137 - Bible in Kiswahili, Revised Union Version 2013

Maombolezo juu ya maangamizi ya Yerusalemu

1 Eze 1:1; Dan 8:2; Isa 24:8; Omb 5:15; Amo 8:10; Ufu 18:22 Kando ya mito ya Babeli ndiko tulikoketi,

Tukalia tulipoikumbuka Sayuni.

2Katika miti iliyo katikati yake

Tulivitundika vinubi vyetu.

3Maana huko waliotuchukua mateka

Walitaka tuwaimbie;

Na waliotuonea walitaka tuwatumbuize;

Tuimbieni baadhi ya nyimbo za Sayuni.

4Twawezaje kuimba wimbo wa BWANA

Katika nchi ya ugeni?

5Nikikusahau, Ee Yerusalemu,

Mkono wangu wa kuume na upooze.

6 Eze 3:26 Ulimi wangu na ugandamane

Na kaakaa la kinywa changu, nisipokukumbuka.

Nisipoikuza Yerusalemu

Zaidi ya furaha yangu iliyo kuu.

7 Omb 4:22; Oba 1:10 Ee BWANA, uwakumbuke wana wa Edomu,

Siku ile Yerusalemu ilipotekwa.

Kwa namna walivyosema, Bomoeni!

Bomoeni hata misingini!

8 Isa 13:1; Ufu 18:6 Ee binti Babeli, uliye karibu na kuangamia,

Heri atakayekupatiliza, ulivyotupatiliza sisi.

9Heri yeye atakayewakamata wadogo wako,

Na kuwaseta wao juu ya mwamba.

Blog
About Us
Message
Site Map

Who We AreWhat We EelieveWhat We Do

Terms of UsePrivacy Notice

2025 by iamachristian.org,Inc All rights reserved.

Home
Gospel
Question
Blog
Help